SHARE

Sauti Ya Watu Lyrics By Nay Wa Mitego | READ

SHARE

Read Sauti Ya Watu Lyrics By Nay Wa Mitego. The song marks another time Nay Wa Mitego has created a socio-political tune meant to highlight challenges facing Tanzanians.

READ ALSO: Read Champion Lyrics By Kontawa Featuring Nay Wa Mitego

Read Sauti Ya Watu Lyrics By Nay Wa Mitego Below:

Hii sio sauti ya kiharakati wala
Ukombozi wa musa na fimbo yake
Bali haya ni maumivu ya mnyonge
Anaye wakilisha walala hoi wenzake
Kwenye kinywa kilichokosa
Pa kusemea hisia zake

Natanguliza samahani kwa wale nitakao wakwaza
Yamenifika hapa nimeshaidwa kunyamaza
Wapo wengi kama mimi wenye sauti kama mimi
Sijui ni ubinafsi hawasemi kama mimi
Anko alisema kwamba tuko uchumi wakati
Haya tudanganyeni tena tupo uchumi wa ngapi

Natanguliza samahani kwa wale nitakao wakwaza
Yamenifika hapa nimeshaidwa kunyamaza
Wapo wengi kama mimi wenye sauti kama mimi
Sijui ni ubinafsi hawasemi kama mimi
Anko alisema kwamba tuko uchumi wakati
Haya tudanganyeni tena tupo uchumi wa ngapi
Wapigaji waliotumbuliwa ndio wamerudi mzigoni

Kameadd kamillion mnataja mabilioni damn
Amna huruma ninyi na sisi masikini
Hivi hio bajeti si mngeweka hospitalini
Na huyu ndio Yule binti aliemaliza chuo
Ila uakka wakazi aliyosomea uko chuo
Hajua atafanya nini amebaki na vyeti vyake
Anajuta alisoma nini si angejiuza ka wenzake
Panya road jina la pili la kijana asiekua na ajira
Na risasi ndio hukumu inamfika hata asie na hatia

Hakuna uafadhali wa maisha vyuma vimezidi kukaza
Mambo yanaharibika na wapinzani wamenyamaza
Kama ulimpenda baba huwezi mwelewa mama
Na kama hukumpenda baba bado utamchukia mama
Yani kumpenda mama na kumchukia baba ni sawa
Kuipenda nyama halafu upendi mchuzi wake
Mmmh, hii ni sauti ya watu
(Na hili giza tunaenda wapi
Tunafanya nini

Tutaishi vipi
Hata mwanga hauonekani)

Ukiona mtoto halii njaa na nyumbani hakuna chakula
We mchunguze vizuri kuna sehemu anakula
Mwambieni ukweli mama hali mbaya sio tandale sio masaki
Kilio cha kila mtu pesa hakuna imefichwa wapi
Siku hizi mpaka vigenge vya nyanya TRA wanataka kodi
Masikini amejichanga vipesa benki anakatwa tozo
Hizo V8 mnazonunua si hela zetu za kodi
Naona mna enjoy kuliko hata walipa kodi
Mnajenga hospitali madawa hakuna

Mnatujengea shule lakini walimu hatuna
Kudanga ndio kimbilio kubwa la dada zetu
Ndio mtaji asiokopeshwa hakatwi tozo wala kodi
Hivi mna akili nyinyi mnashauri tujiajiri
Wakati nyinyi wenyewe mpaka sasa mmeajiriwa
Achieni nafasi zenu na nyinyi mkajiajiri
Hapo ndipo nitapoamini kweri nyie washauri wazuri
Kati ya mtawala na mpinzani hapa muogo nani

Mtawala aliekataza mikutano isifanyike
Au mpinzani asieifanya na anajua ni haki yake
Mmmh, hii ni sauti ya watu

Na hili giza tunaenda wapi
Tunafanya nini
Tutaishi vipi
Hata mwanga hauonekani

Related

ADVERTISEMENT