SHARE

Read Nipeni Maua Yangu Lyrics By Roma Mkatoliki Ft Abiudi

SHARE

Read Nipeni Maua Yangu Lyrics By Roma Mkatoliki Ft Abiudi. The song marks another time Roma Mkatoliki has scored a hit song.

READ ALSO: VIDEO: Roma ft. One Six - Mkombozi

Read Nipeni Maua Yangu Lyrics By Roma Mkatoliki Ft Abiudi Here:

Tumekumisi Roma 

Rudi Nyumbani 

Uwatetee Wanyonge ndugu zako 

Uwakumbushe 

Sasa sijui nianzie wapi kifuani nimebeba mengi 

Na sitotenda haki nisiposema hiki sipendi 

Hiki napenda kile sitaki mambo ya kishenzi 

Tanzania haijaezekwa bati na wamekula pesa ya ujenzi 

Yaani nchi wanaifanya mti mjenzi anauona mbao 

Ndege ataona makazi mkulima ataona mazao 

Mganga atauona dawa na mpishi atauona kuni 

Ataemiliki mwenye power sisi atatusagia kunguni 

Na ukisema hawatufai wanakuumiza uwe mpole 

Yaani wanaangua papai kwa kutumia gobole 

Mnatumia nguvu kubwa kwenye mambo madogo 

Jeshi gani mpaka leo mmeshindwa kumjua kigogo 

Tukiongelea kutekwa eti tunarudia ajenda 

Hamjibu mnakwepa mbona mama anarudia kilemba 

Nchi gani raia akihoji mnasema anakosoa 

Na akikosoa anatukana serikali hii sio poa

Haya basi tuseme mko sawa na mna nia nzuri na sisi 

Mbona vyuma vimekaza halafu mama anaificha grease 

Mara mkapandisha tozo kampeni mkono hatuwaungi 

Si tulihoji mkajibu kwa dharau tuhamie Burundi 

Tatizo mkishaapishwa tu mnawaza uchaguzi ujao 

Hamuwazi njia mbadala ya kumlinda mkulima na mazao 

Sasa Iringa si tuna maitu halafu tuspick twaagiza china 

Manaake hapo kwanza ncheke yaani bongo kikubwa uzima 

Sa mnatuambia tujiajiri mbona nyinyi hamkujiajiri 

Okay nikupe bodacyangu kisha we unipe uwaziri 

Nikukabidhi vyeti vyangu hangaika navyo mwezi mmoja 

Niko pale nakujgoja uje tuongee lugha moja 

Mi sio CCM sio Chadema hili niliweke wazi 

Ila ukiweka CCM na Andazi ntachagua Andazi 

Simuamini mtawala na mpinzani simsadiki 

Maana wanaendelea kukatika huku deejay kauzima Mziki 

Na inaniuma kuona msomi wa degree tatu 

Nashindwa kumpa ajira sasa anauza nyanya karatu 

Sasa sijui mtaniua nikimshikia mama shilingi 

Maana hata inyeshe mvua mnasema anaupiga mwingi 

Na ninamkubali na nitamng’ata sikio kama hujui 

Wanaomkosoa ndo wanampenda wanaomsifia ndo maadui 

Ili wapate teuzi ndo wanamlamba miguu 

Wakimpamba hawamsaidii Amiri Jeshi Mkuu 

Tunakupenda Roma Tunakumiss Roma 

Rudi Nyumbani Roma Utusemee 

Tunakupenda Baba Tunakumiss Mwana 

Tunakukumbuka sana 

Hivi hamjasikia tetesi kuwa remote iko msoga 

Si huku mageng imedoda magogoni imenona 

Watu tatu ndani ya track moja wamekalia kigoda 

Ngolo Kante anampa Mbape cross anafunga Pogba 

Hii nchi ina wenye nchi walanchi na wananchi 

Na kuendelea kuwachagua ni kwenda na mchanga mbichi 

Tuwajaribu wapinzani watawala si wameshapata 

Ugoro umewaingia puani sasa ona wanapiga chafya 

Wanatumia dollar kubaki kuongoza dola 

Watawafunga watapora wataua watahonga vijora 

Karatasi tunaibiwa za kura kwenye sanduku 

Kwa hiyo mnatuonyesha ziwa huku mmeziziba chuchu 

Okay kura ziko 300 na kuna watu mia kwa jimbo 

Na kituoni hakukua na watu halafu wameshinda kwa kishindo 

Sa kama Askofu mfufua watu ameiba kura za wapinzani 

Je atashindwa kuiba sadaka za kura kanisani 

Hii ni gani mchungaji akitaka gari twamchangia 

Muumini akitaka gari anaombewa tunamsalia 

Sa mchungaji tusimpe pesa tumuombeevna yeye pia 

Tukae pale tusubiri miujiza ya wagalatia 

Wabunge wengi mlishinda kwa hisani ya mwendazake 

Mkipatacho muende Chato mkumbuke hata ndugu zake 

Jimbo hili haliendelei cause mmemchagua mpinzani 

Haya sasa mmeshinda kote fauluni huo mtihani 

Turuhusu siasa za amani turudi zile enzi zetu 

Uchaguzi sio siku moja ni mchakato wa muda mrefu 

Mikutano ya nje na ndani ndo tunaimarisha chama 

Daily mtulishe majani halafu sikukuu mtupe shawarma 

Keki ya taifa ni kubwa tuache siasa za risasi 

Mnawaonea wakishika dola watalipa kisasi 

Tulipotoka ni mbali siasa za mwendazake 

Msirudi msilale chali huku mnatutemea mate

Na BASATA msikie hili msije fungia huu wimbo 

Kichwa kisicho na akili ni mzigo kwa shingo 

Sawa tulinde maaduli ila tusiue wabunifu 

Mtupende tunaokosoa kama mpendavyo wanaosifu 

Wengine wamekuwa viongozi na mliwaona tu marapper 

Hiphop ni mkombozi na sauti isiyo na mipaka 

Ushauliza kwanini bega lipo karibu na kwapa 

Usiondoke baki hapa usikie verse inayofuata 

Tunakupenda Roma Tunakumiss Roma 

Rudi Nyumbani Roma Utusemee 

Tunakupenda Baba Tunakumiss Mwana 

Tunakukumbuka sana 

Nawashangaa vijana warembo na watanashati na nusu 

Wanaosema bila mlengo eti siasa haiwahusu 

Mwanasiasa anaweza amua tu na ukalala mahabusu 

Mnakosea wadogo zangu na kamwe sitoruhusu 

Siasa ndo inaamua sukari iuzwe shingapi 

Na inapanga kaliua ni wapi wajenge zahanati 

Na ijue tofauti ya mwanasiasa na mwanaharakati 

Mmoja ndo mzalendo mwingine maslahi binafsi 

Ntawafundisha kitu kabla hajawika jogoo alfajiri

Pesa unayonunua maduta mkate unaolipa bili 

Hoja yake inamlipa Raisi Polisi Mbunge Waziri 

So una haki ya kuwakosoa maana we ndo umewaaajiri 

Tatizo hatuna ujasiri na akili tumekaza fuvu 

Vipi nitafuzu kichwa suzuki engine ya Isuzu 

Anayechelewesha msafara siku zote ni ng’ombe wa mbele 

Ila anachapwa wa nyuma na ndo anayepiga kelele

Na mjenga katiba mpya sio BAWACHA wala BAVICHA 

Eti wabonngo maji sio katiba mnawaficha 

Haya sasa hayo maji yako wapi mbona hamuongei 

Uko wapi umeme mmebugia kiazi cha mtoto

Mdomo unacheza sebene 

Katiba iliyopo ni bora ipa ni bora kwa watawala 

Ukipinga wanakupa keai na hauna hela kibatala

Kwa mwamvulu wa maendeleo wanahairisha mchakato 

Mbona mkoloni alijenga miundombinu yote hapo 

Na ili nchi iendelee inahitaji vitu vinne tu 

Uongozi bora, siasa sadi, Ardhi na watu 

Yanga na Simba ni wapinzani ila sio kwamba hawapatani 

Maji yanayotoka mto msimbazi ndo yanayojaza jangwani 

Na hiyo ndo amani tuitakayo sisi sio vurugu 

Tunataka kuona Januari anamgongea fegi sugu 

Hakika naacha glasi ya Bapa mezani anaenda msalani 

Anamuachia mwigulu anarudi na anakunywa kwa amani 

Na sio utani msipojifunza hapa ndo basi tena 

Aliyesema aomgezewe muda bungeni ndo ameaga mapema 

Wakamlisha asali kwa kisu akalamba akamwaga wino 

Tangulia na dereva barua utaikuta chamwino 

Mi nitakufa mimi ila ngoma zangu zitaishi 

Na mtakuja na mashada siku yangu ya mazishi 

Nipeni maua yangu niyanuse angali nipo hai 

Nikiondoka mnikumbuke msilie bali mfurahi 

Tunakupenda Roma Tunakumiss Roma 

Rudi Nyumbani Roma Utusemee 

Tunakupenda Baba Tunakumiss Mwana 

Tunakukumbuka sana 

Related

ADVERTISEMENT