SHARE

Nitasimama Lyrics by Roma Mkatoliki

SHARE

Roma Mkatoliki Lyrics

Read Nitasimama Lyrics by Roma Mkatoliki. The song is well received by fans in Tanzania and beyond.

READ ALSO: Paka Na Panya (Derby) Lyrics by Roma Mkatoliki featuring Latifah

Read Nitasimama Lyrics by Roma Mkatoliki below:

Unazaliwa kwenye familia duni ya kifukara
Nyumbani hali mbaya kichumi msosi wa duara
Ugali saizi ya ngumi na mpo saba hamjala
Hata kipande cha sabuni kumudu usifanye masihara
Sayansi ya Mungu utaikufuru kisa njaa
Maana huwezi chagua aina ya mzazi atakayekuzaa
Jirani kazaliwa na Waziri wewe mama yako kichaa
Baba mlevi alafu konda wa daladala tu kibaha

Daah usikate tamaa naimute snare upate hamasa
We ndo wa kuibadili sura ya familia kuanzia sasa
Na unaweza mbona wameweza waliotangulia
Na wana kichwa kama wewe hawana mkono wa bandia
Na pia skia mzazi maisha haya usichague kazi
Na nikuweke wazi usiskize wataoku-judge
Kuna dada baadhi wanaamini wao wana hadhi
Hawaamini wana kazi na wala nini hawawazi
That's nonsense born poor die poor
No offense acha niwajuze msichokijua
Tuna akili zaidi yenu ila mna nguvu zaidi yetu
Na nguvu mtaji wa akili hadi hapo hamjaliona gepu

Sasa mnakwama wapi ingiaa mzigoni amka dada maisha haya usitegemee ndugu atakupa msaada
Tafuta chako haina furaha hiyo pesa manyanyaso
Na kuna raha kula pesa yako uliyoitolea jasho

Nitasimama tena Nitasimama tena
Nna imani Nna Imani
Utasimama tena Utasimama tena
Nna imani Nna Imani

Get Fresh updates as they drop via Twitter and Facebook

Related

ADVERTISEMENT