SHARE

Calling Lyrics by Professor Jay Ft Ali Kiba

SHARE

Professor Jay Lyrics

Read and sing aloud Calling Lyrics by Professor Jay Ft Ali Kiba. The song has been well-received by fans in Tanzania.

EP cover

Calling Lyrics by Professor Jay Ft Ali Kiba

Mmmh!!

Yeap!!!

Yeah

Professor j foundation

Bin laden

Amekuwa mkiwa, amegunikwa na unyonge

mwenye ukiwa wa njiwa, koo limekabwa na donge

Alikuwa na furaa, mama yake alipokuwepo

Gafla mama akazima kama ushumaa kwenye upepo

Kwenye umri mdogo hakuona pengo lolote

Zaidi ya kuchezacheza, bila ya kujua chochote

Adhabu ilianza alipokuja mama wa Kambo

mateso na maneno kila alipofanya jambo

Yeye alibaguliwa, hakupendwa kama wengine

alipewa kazi ngumu sana utadhani mashine

kutwa anashunda Njaa, moyon Hana furaa

ukimwangalia usoni amefubaa, ameshakata tamaa

haoni Tena sababu ya kuishi na ndugu zake

kutwa Yuko peke yake, akimlilia mama ake

Hana kosa lolote huyu malaika wa mungu

Hajatenda jambo baya, mnamwamuru atubu

She is calling ooh calling

Kwa waliopitia shida aaah,

kwani haya maisha, ipo siku yataisha

ipo na

usikate tamaa aaah, kwani hata mbuyuu ulianza kama mchichaa

jikaze tutafika, she is calling

Alipenda kusoma elimu ije kumsaidia

tabu alizozipata aliona azivumilie aliupenda urubani

ila elimu ikawa ndoto, shuleni kama vitani yaani amani amani ndani ya moto

akienda shuleni wenzake wanamcheka

nguo zimechakaa nafsi yake inakereka

alikuwa kama mtumishi asiyelipwa Mshahara

ilibidi afanye kazi aweze kulala

alipewa kazi ngumu tofaut na umri wake

ilibidi aongeze juhudi Ili aokoe nafsi yake

akifanya kosa dogo mikono inachomwa moto

hakika walimkomaza ilihali umri Bado mdogo

alimwomba mola wake ampunguzie mateso

Ili siku ipite walau waione kesho, mara nyingi alitoroka na kukimbilia mtaan

jua lake mvua yake analala barabarani

She is calling ooh calling

Kwa waliopitia shida aaah

kwani haya maisha, ipo siku yataisha

isha na

usikate tamaa aaah, kwani hata mbuyuu ulianza kama mchichaa

jikaze tutafika,

fika

she is calling

mungu akamsikia, akavumilia yote

maana hata mkosaji daima hakosi vyote

akihitimu primary secondary na chuo

Kwa kuwa aliamini elimu ndiyo ufunguo

muda ukazidi kwenda akapata kazi nzuri

akachapa kazi akapata pesa na umashuhuri

aliishi vizuri na Watu mtaan kwake

walimuona kama kiongozi Bora Kwa moyo wake

alipoona yatima maumivu alijitonesha

alikumbuka alivyopata tabu kujisomesha

alilipa wema hakuwa mtu wa visa

aliwasamehe mama wa Kambo na baba mzazi

aliwasomesha wadogo zake wapate elimu

akasaidia wazee mahitaji yote muhimu

watoto mnaowatesa ndio watawasaidia

mtoto wa mwenzio ni wako na kiongozi wa Tanzania

(baadae)

She is calling ooh calling

Kwa waliopitia shida aaah

kwani haya maisha, ipo siku yataisha

isha na

usikate tamaa aaah, kwani hata mbuyuu ulianza kama mchichaa

jikaze tutafika,

fika

is calling

ooh calling

Kwa waliopitia shida aaah

kwani haya maisha, ipo siku yataisha

isha na

usikate tamaa aaah, kwani hata mbuyuu ulianza kama mchichaa

jikaze tutafika,

fika

she is calling

instrumental

tongwa records

bin laden

Read Other Latest Song Lyrics Here

Get Fresh updates as they drop via Twitter and Facebook

Related

ADVERTISEMENT